Ijumaa, 27 Desemba 2013

UJANA ULIO SALAMA



KANUNI  ZA  KUTUNZA  UJANA  WAKO;

Ujana kama lulu ambayo inathamani kubwa sana katika dunia ya sasa hivyo inahitajika sana kutunzwa ili iweze kuendelea kuwa bora sana na yenye manufaa katika kizazi chote. Kama inavyojulikana wazi kitu chochote kisipotunzwa basi kunahali ya kuharibika ambayo inakaribia na isipoangaliwa jambo baya linaweza kupelekea kutia nanga katika ujana.

Jua kama usipo jitambua na kujithamini hakuna mtu atachukua nafasi yako na kufanya yale uliyotakiwa kujifanyia wewe binafsi.

Unaweza kutamani kuwa kijana unaye jitunza lakini usipofuata kanuni ambazo zinazo kuwezesha kujitunza hauwezi kuwa kijana wa maana kwa Mungu na kwa wanadamu na hatimae dunia ikafaidika kupitia wewe.

Kila namna unatamani kuwa lazima pawepo na namna ya kukufanya wewe kuwa mtu husika mathalani ukita kuwa mwalimu mzuri kuna kanuni za kukufanya uwe hivyo na vilevile ukitaka kuwa mwanafunzi bora lazima kuna kanuni/namna ya kukufanya mwanafunzi bora unaweza ukatamani kuwa mtu yeyote kwa namna ya mtazamo wako ulivyo lakini kama ujafuata kanuni zilizowekwa kamwe hauwezi kuwa vile unatamani.

Hivyo unaweza kutamani sana lakini kama tu hautafwata kanuni kamwe hauwezi kufika pale unafikiria hivyo
 KUTAMANI  BILA  KUFUATA  KANUNI  HAKUNA  KITU KITAKACHOFANYIKA.

Kanuni za kutunza ujana wako katika kiwango cha Mungu;

i.kumpenda Mungu

ii.pendo la Mungu kuchukua nafasi ndani yako

iii.usiogope

iv.macho ya rohoni

v.ukaribu

vi.kumtazama Mungu

vii.kujitunza

viii.uaminifu

ix.usijiamini

x.maongezi


Prepared by ;
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                   
                     Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com             

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni