KIJANA NI NANI
NA AFANYE YA
PI ILI KUJIKOMBOA?
Kijana ni hatua ya kujivunia sana kwani ni wakati wa kutambua na kuona mwanga sahihi wa maisha na kutambua kwanini upo na unahitaji nini ili uweze kuwa wa maana zaidi sana. Tuta kwenda kuangalia kwa namna ambayo itatusaidia kujitambua kuwa kijana ni nani na kuanza sawasawa na ulivyoelewa kwa pamoja tukielimishana tunaweza kufika mahali pa juu zaidi ambapo tunaweza kung’ara.
Ujana ni bidhaa adimu sana na ghali sana kwakua
haiko hatua ambayo unaweza kuilinganisha na hatua hii kwakua ni ya kipekee na
yatofauti sana.
Kijana
ni nani?
Yoshua
21:18
kutokana na takwimu na maelezo ya watu mbalimbali
wamejaribu kuelezea maana ya kijana katika namna mbalimbali mathalani muonekano
wa kijana, nguvu katika utendaji, mawazo ya kijana na uchumi wa mtu aliye
kijana na hata matumizi wa huo uchumi wa mtu huyo anaitwa kijana.
Kutokana na maelezo hayo mbalimbali lakini mimi
nitajikita katika umri ambao tunaweza kupata maana ya kijana ni mtu aliye na
umri ulioanzia 18 hadi 45 ni hatua ya kati kutoka utoto kwenda utu uzima.
Kijana kama kijana jua kwamba unalokusudi ambalo
linabidi utoke na kwenda kwa jamii kubwa nao kupata kitu ambacho kitawafanya wa
kukumbuke na waone fahari ya wewe kuwa pamoja nao.
Vijina katika dunia tuliyonayo ndio wanaoshangaza
ulimwengu na kuufanya vile wanavyo taka wako vijana wengi wamejiingiza katika
biashara ya madawa ya kulevya na wengine kujiingiza katika vitendo vya ngono
katika kujirahishia maisha yao na wengine kufanya vitendo vya uhalifu kama vile
ubakaji,wizi(ujambazi) na hata wengine kushiki katika kujitoa mwanga kuwatayari
kujitoa kwa ajili ya maisha yao na mengine mengi ambayo vijana wamejiingiza
katika hayo na hatimaye kupelekea kuwa katika majanga mbalimbali kama vile
kifo.
Dunia ya sasa hakuna mitu mzuri ambaye anatafutwa
kwa hali na mali kama kijana kwakua imefika nyakati kusema kwamba dunia ndio
muhimiri wa dunia kupitia hao wanaweza kuifanya dunia kuwa katika hali tofauti
ambayo watakayoikusudia katika hali njema au mbaya inawategemea wao.
Imekuwa ni kilio cha watu wengi hasa wazee kwa kuona
vijana wanaangamia katika majanga yanayoikabili dunia ya sasa imekuwa zaidi ya
tatizo kwakua kila majanga yanayotokea basi lazima kwa kiasi kikubwa wahusishwe
watu ambao hasa ni vijana ingawa kwa kiasi
kikubwa hili kundi la vijana halifaidiki ipasavyo lakini linatumika sana huku
likiendelea kuteketea.
Kusema ukweli kilio hiki sio cha wazazi au wazee tu
bali hata Mungu mwenyewe ni anasikia maumivu makubwa kutikana hile hazina iliyo
ndani ya mwanadam ambayo aliiweka mwenyewe kwa ajili ya kusudi lake lakini
matokeo yake ile hazina inatumika kwa ajili kuubomoa ule ufalme wake anakosa
furaha ya kujivunia vijana ambayo walitakiwa wabebe sura yake,nguvu zake,mmlaka
yake hapa duniani kwa kufanya yaliyo yake.
Japo katika hali hii utaitole hesabu ya nguvu na
uwezo binafsi aliyokupa Mungu umeitumiaje wakati ambao hakuta kuwa na wakati
wakurudi nyuma tena.
I saya 47:8-11,15
I wakorintho 7:32
Maombolezo 3:27
Vijana wengi wamepotelea katika maisha ambayo hatima
yake ni kupotea kabisa pasipo matumaini mema mbayo Mungu alikusudia ndani ya
neno lake Mungu anasema kwamba afurahishwi na kifo cha mwenye dhmbi, kwakua
hana matarajio mabaya kwa mwanadamu yeyote mbaye yeye Mungu alimkusudia.
Ezekieli 33:11
“Maana nayajua mawazo ninayowawazia
ninyi,asema BWANA , ni mawazo ya amani wala sio mabaya kuwapa ninyi tumaini
siku zenu za mwisho.”
Yeremia
29:11
Mungu ajaweka jehanamu kwa ajili ya kuangamiza
maisha ya mwanadamu bali ilikuwa ni kwa ajili ya shetani na malaika wote walio
muasi na sio kwa ajili ya mwanadamu hivyo Mungu umia sana kuona watu wakienenda
na hatima yao kuwa sawa na shetani anapokwenda.
Japo kuna maneno ambayo wanadamu wanasema kuwa Mungu
ametuacha ukweli ni kwamba ni sisi ndio tulio muacha Mungu kwakujua au
kutokujua.
Mungu akumtengeza kijana kwa namna alivyo kwa kusudi
kwamba aje ateseke naye Mungu afurahie kwa kuteseka kwako kamwe hilo silo
kusudi la Mungu lisivyokuwa kusudi la mzazi kwa mwanae aliye mzaa.
Katika hali ya uhalisia ni kweli kwamba sio utoto au
ujana wala utuuzima waeza kukuwezesha uweze kufanya upasavyo bali ni Mungu tu
ndani yako akuwezeshe WOKOVU HALISI.
Yohana
15:5
Ukweli utakapo ujenga ujana katika misingi mizuri ni
wazi hapo ndipo utaona ustawi mzuri wa Ki Mungu ndani ya hatua zinazofuata
pasipo upingamizi wowote utakao kushinda bali vyote vinakuwa ni rahisi
kufanyika kwa Mungu anatembea kupitia wewe.
Na ndipo hapo utaweza kustarehe katika ujana wako na
kufurahia maisha yako yote kwakua furaha yako itakuwa ikilindwa na Mungu.
Yohana 21:18
Ujana ni hatua ambayo akili inapevuka na kuuhitaji
kujua vitu vingi na vitu vingine ambavyo alikuwa mwanzo anakosa uhuru kuvijua
basi tumia fursa hiyo kujua zaidi sana kuhusu Mungu ili upone na dunia hii
iliyojaa kila haina ya matatizo.
Wakolosai 2:23
Yeremia 3:4-5
Prepared by ;
Nelson, Cothey – 0764 018
535 or cotheyn@yahoo.com
Katiti, James - 0713 398 042
or james.adili19@gmail.com
Ni vizuri tuseme kuwa tunakupenda……………siku
njema!!